Waziri
wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) amewataka watumishi wa
Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake kuwahudumia wananchi kwa
uadilifu ili kujenga uaminifu kwa wananchi na Serikali yao.
Dkt
Mpango aliyasema hayo alipotembelea banda la Wizara ya Fedha na Mipango katika
viwanja vya maonesho Nanenane katika eneo la Ngongo mkoani Lindi.
Alisema
kuwa Wizara ya Fedha na Mipango inategemewa na wananchi wengi hivyo ni vyema
wahudumiwe vizuripamoja na kutoa elimu kwa umma vya kutosha ili waweze kuelewa
na kuridhika na huduma zinazotolewa na wizara.
“Tujitahidi
kuwaelezea wananchi juu ya kazi na huduma zetu ili waweze kuzitumia kwa manufaa
yao na Taifa kwa ujumla na tuweze kufikia uchumi wa viwanda kama lengo la
Serikali ya Awamu ya Tano ilivyojipangia ” Alisisitiza Dkt. Mpango.
Kauli
mbiu ya maonesho ya Nanenane mwaka huu ambayo ni ya 24 kufanyika kitaifa huku
yakifanyika mwaka wan ne mfululizo mkoani Lindi inasema “Zalisha kwa tija mazao
ya kilimo, mifugo na uvuvi ili kufikia uchumi wa kati”.
Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha
na Mipango
Ngongo Lindi
Post a Comment
karibu kwa maoni