0
Kampuni ya DSTV Tanzania imemdhamini mshindi wa tano mtanzania Alphonce Felix Singu kutoka Singida mashindano ya riadha Olympic mbio ndefu yaliyomalizika mwaka huu miezi michache iliyopita huko Rio de Janeiro nchini Brazil kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Singu ameushukuru uongozi wa DSTV kwa kumsimamia huku akiwataka wengine wajitokeze kusaidia wana riadha amabao wapo wengi hawana wafadhili.
Mwanariadha huyo ameeleza kuwa mbinu anazotumia katika riadha na kupata ushindi ni mazoezi ya mara kwa mara bila kukata tamaa akiwapa moyo wanaraiadha wenzake kujituma biloa kuchoka kwani mafanikio katika riadha ni makubwa.
'Sisi watu wa riadha kupata msaada ni ngumu kidogo cha kufanya ni sisi kujituma,ukishafanya jitihada watu watakuja wenyewe watakufuata"alisema Singu.
Alex Singu mshindi namba tano.
DSTV wanaorusha michezo mbali mbali ya kimataifa ikiwemo ile maarufu ya ligi kuu soka ya UINGEREZA EPL wameamua kumsimamia Singu kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuzidi kutoa motisha na kuwapa moyo washiriki wengine wa Mashindano kama hayo.
Sambamba na hilo Meneja wa DSTV Tanzania Salum Salum amemzawadia King'amuzi cha DSTV bingwa wa riadha Tanzania anaetokea mkoani Manyara Ismail Juma katika mshindano mbalimbali,mashindano ya taifa 2016 katika mita 5000,mita 10000,Kilimanjaro half Marathon mshindi namba moja,CROSS COUNTRY iliyofanyika nchini CHINA mwaka 2015 alishika namba tisa [9] na kuipeperusha bendera ya Tanzania.
Salum amemkabidhi Kingamuzi hicho pamoja na Dish lake ili aendelee kufuatila michezo mbali mbali duniani huku wakimtaka aongeze juhudi zaidi..
"Kupitia riadha nimejenga na ninaisaidia familia yangu lakini pia imenisaidia kuzijua nchi mbalimbali duniani na kupata heshima'alisema Ismail Juma
Ismail ameshiriki mashindano makubwa nchini Brazil alikuwa wa kwanza mwaka 2012 Kilomita 10 na kilomita 21, miezi mitatu aliishi Brazil, China 2015,Nigeraia 2016 alishika nafasi nya pili Kilomita 10.
Ismail anasema ugumu anaokutana nao katika mazoezi ni kukosa lishe na matunda ambayo ni muhimu kwa afya.
Meneja Wa DSTV amesema kuwa kuona ni kuamini hivyo wameamua kumleta Singu kama balozi Manyara  kwa kuwa ndipo chimbuko la wanariadha wengi ili kuwapa moyo ziadi wengine na kueleza kuwa wamevutiwa na kiwango cha Ismail Juma.
Meneja  wa Kampuni ya DSTV Tanzania,Salum Salum
Naye Singu amekubali kiwango cha Ismail na kukiri kuwa alishiriki nae mwaka jana katika mashindano ya riadha yanayojulikana kama Cross Country yaliyofanyika nchini China yeye akishika nafasi ya 49 huku Ismail akishika nafasi ya 9.


Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top