0
Hatimaye kiingilio katika usiku wa Baraka da Prince kimetajwa itakuwa ni shilingi 7000 kwa kila kichwa huku mlangoni kwa watakaoingia wakipatiwa kopo kubwa lililojaa ubuyu wa rangi nyekundu.
Akizungumza na Blog hii mtayarishaji wa Burudani mjini Babati Said Kopwe CHINI YA KAMPUNI YAKE ya Side entartainment akishirikiana na Good Talent Entertainment amesema kuwa watakaoingia wote watahakikishiwa usalama wao pamoja na vyombo vya usafiri watakavyokuja nao.
Baraka dar Prince anatarajiwa kushuka mjini Babati leo tarehe 23 februari kwa ajili ya kuwapa raha mashabiki wa mziki wake mjini Babati na vitongoji vyake hapo kesho katika ukumbi wa Club Lavista kuanzia saa tatu usiku.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top