0


Naibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Salumu ametangaza kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, NECTA limesitisha mpango wa kuwafanyia mtihani wa udahili wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika shule za sekondari za serikali.
Usitishaji huo umetokana na wakuu wa shule za serikali kushindwa kukidhi baadhi ya masharti yaliyotolewa na NECTA, mazingira yaliyopelekea NECTA kusitisha zoezi la udahili wa wanafunzi hao wanatakiwa kujiung na masomo kidato cha kwanza.
Ambapo NACTE iliwataka wakuu wa shule kuhakikisha mtihani huo unafanyika kwa wanafunzi wote wa shule za serikali siku moja na muda uliopingwa, pia masharti yaliwalazimu wakuu wa shule za serikali kuwasilisha orodha ya majina ya wanafunzi kwa maofisa elimu wa mikoa na wilaya ili yatumwe NECTA.
Mazungumzo hayo yalifanyika juzi kwenye kikao cha wadau wa sekta ya elimu Mkoa wa Morogoro alipokuwa akihitimisha mada yake kwa wajumbe wa kikao hicho kilichoongozwa na mkuu wa mkoa huo, Dk Stephen Kebwe.
“Necta imewasiliana na wahusika kwa barua rasmi ya kusitisha mtihani huo ambao ulipangwa ufanyike Februari 28, mwaka huu na wanafunzi wote waliopangiwa kidato cha kwanza shule mbalimbali za serikali zikiwemo za bweni, waendelee na masomo kama yalivyopangwa,” alieleza Naibu Katibu Mtendaji wa Necta.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top