Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania limesema
kuwa linamuunga mkono Rais DKT.John Magufuli kwa kazi yake nzuri
anayoifanya ya kuimarisha uchumi wa nchi na kuwafichua wahujumu uchumi.
Kauli hiyo imetolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Mark Malekana wakati wa Ibada maalum ya kanisa hilo, ambapo pia kumefanyika uzinduzi wa Programu Mpya ya kuwafikishia injili Watanzania wote.
Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chalya Julius kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makala, amesema serikali itaendelea kuimarisha amani ili waumini wote wa dini mbalimbali waendelee kuabudu kwa amani na utulivu.
Aidha waumini hao pia wametoa huduma ya afya, ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwaajili ya kuongeza akiba ya damu nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Mark Malekana wakati wa Ibada maalum ya kanisa hilo, ambapo pia kumefanyika uzinduzi wa Programu Mpya ya kuwafikishia injili Watanzania wote.
Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chalya Julius kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makala, amesema serikali itaendelea kuimarisha amani ili waumini wote wa dini mbalimbali waendelee kuabudu kwa amani na utulivu.
Aidha waumini hao pia wametoa huduma ya afya, ikiwa ni pamoja na kujitolea damu kwaajili ya kuongeza akiba ya damu nchini.
Post a Comment
karibu kwa maoni