Mjumbe wa kamati kuu ya chama
kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, Edward Lowassa amefichua
kuwa Rais John Magufuli alimuomba arejee chama tawala cha CCM wakati wa
mazungumzo yao juma lililopita .
Katika taarifa iliyotolewa na
Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, kwa waandishi wa habari
Lowassa ameeleza "ujumbe wa Rasi Magufuli ulikuwa kunishawishi kutaka
nirejee CCM, suala ambalo sikukubaliana nalo na nilimueleza Rais ya
kwamba uamuzi wangu wa kukihama chama hicho na kujiunga na CHADEMA
haukuwa wa kubahatisha"Wiki iliopita, kiongozi huyo wa upinzani nchini Tanzania, ambaye pia ni Waziri mkuu wa zamani, alikutana na Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli Ikulu na kumsifu sana kwa kazi anayoifanya.
Ni hatua ambayo iliwashangaza wengi kwani si kawaida kwa kiongozi huyo kumsifu Rais Magufuli kwani kwa muda amekuwa akikosoa utawala wake.
Bw Lowassa aliwania urais kupitia chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015 lakini akashindwa na Dkt Magufuli aliyewania kupitia Chama cha Mapinduzi.
Post a Comment
karibu kwa maoni