Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) limeiteua
Tanzania kufanyia mkutano wake mkuu wa kila mwaka utakaoshirikisha
mataifa 19 ambayo ni wanachama wa Shirikisho hilo.
Mkutano
huo mkubwa wa Kihistoria umepangwa kufanyika Februari 22 katika Ukumbi
wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
na kuongozwa na rais wa shirikisho hilo, Giani Infantino.Baadhi ya agenda zinazotarajiwa kujadiliwa kwenye mkutano huo utoaji wa fedha za Fifa kwa ajili ya maendeleo ya soka na changamoto za usajili kwa njia ya mtandao ujulikanao kwa kiingereza Transfer Matching System.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF, Wallace Karia ameipongeza Fifa kwa kuichagua Tanzania kuandaa mkutano huo na kwamba hiyo ni heshima kwa Tanzania.
Ofisa wa mawasiliano kutoka kitengo cha habari, TFF, Clifford Ndimbo amesema wageni watakaohudhuria mkutano huo wataanza kuwasili Tanzania Februari, 20.
Mataifa yatakayoshiriki mkutano huo ni Tanzania (mwenyeji), Algeria, Mali, Morocco, Burkinafaso, Angola, Niger, Bahrain, Palestina na Saud Arabia. Mengine ni Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ivory Coast, Tunisia, Bermuda, Monserrat, St Lucia, Visiwa vya US Virgin, Maldives na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Post a Comment
karibu kwa maoni