Aliyekuwa
Diwani wa kata ya Bagara Babati mjini mkoani Manyara kupirtia chama cha
Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA] Nichodem Bonifasi maarufu kama Nyeusi
amejiunga na chama cha Mapinduzi.
Akitangaza
kujiunga na Ccm leo Nyeusi amesema utendaji kazi wa rais John Pombe Magufuli
uliotukuka ndio uliomfanya ajiunge na chama hicho huku akiahidi kuendelea
kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika kutekeleza ilani ya Chama cha
Mapinduzi.
Aidha amesema
bado anao uwezo wa kuwatetea wakazi wa kata ya Bagara na ameomba apewe ruksa
kupitia chama cha mapinduzi na sio diwani wa Halmashauri ya mji wa Babati, kufanya ziara na kumtangaza rais Magufuli.
Diwani huyo
ameomba uongozi wa ccm umpatie ulinzi kwa maelezo kuwa kuna watu wanamfuatilia.
Naye katibu wa
siasa na uenezi Ccm mkoa wa Manyara Jacob Aloyce Siay amesema jambo hilo la
diwani huyo wa kata ya Bagara kujiunga CCM ni la kishujaa na la kupongezwa.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa vijana ccm mkoa wa Manyara Mosses Method Komba amesema
wamempokea kwa mikono miwili diwani huyo.
Diwani huyo
juzi katika baraza la madiwani linaloongozwa na Mwenyekiti Mohamedi Kibiki
alionekana akiungana na madiwani wa Ccm katika sakata la kukikabidhi chama cha
Mapinduzi Kituo cha Mabasi cha Babati.,madiwani wa Ccm walikataa suala
kujadiliwa huku chadema wakitaka lijadiliwe.
Halmashauri
ya mji wa Babati inaongozwa na wabunge wa Chadema ambao kwa idadi yao kwa sasa
wapo wanne baada ya Diwani wa kata ya Bagara Nikodem Alfonsi kuondoka.
Post a Comment
karibu kwa maoni