Aliyekuwa
Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (CDM) jimbo la Siha Mkoani Kilimanjaro Elvis Mosi amesema
kuwa ana mpango wa kufungua kesi Mahakamani kupinga matokeo ya
uchaguzi yaliyompa ushindi Dr Godwin Molel
wa CCM kwa madai kuwa taratibu na kanuni za uchaguzi zilikiukwa
hivyo anatarajia kulifikisha suala hilo Mahakamani.
Mosi ambaye alipata kura 5905 dhidi ya kura 25611 za Dr. Molel amesema,
wanakusanya ushahidi wa kutosha ambao utaiwezesha Mahakama kutengua matokeo
hayo na uchaguzi kurudiwa.
Akizungumza
na waandishi wa habari nyumbani kwake Sanya Juu, Mosi amezitaja baadhi ya taratibu
zilizokiukwa ni pamoja na kubadilisha matokeo ya kura zake katika vituo na
kupewa Dr. Molel jambo ambalo lilimfanya asisaini fomu za matokeo.
Post a Comment
karibu kwa maoni