0
Mcheza
filamu, Elizabeth Michael maarufu Lulu amebadilishwa kifungo na sasa
atatumikia adhabu hiyo akiwa nje yaani ‘kifungo cha nje’.




Lulu,
alishtakiwa kwa kesi ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa muigizaji
maarufu wa filamu nchini na nje ya nchi, Steven Kanumba ambaye pia
alikuwa mpenzi wake.


 
Ofisa
Habari wa Jeshi la Magereza, Lucas Mboje amesema Lulu amebadilishiwa
adhabu  na atatumikia kifungo cha nje kwa amri ya Mahakama Kuu ya
Tanzania, Dar es Salaam.




“Lulu
amebadilishiwa adhabu na ameachiwa juzi Jumamosi kati ya saa 2 hadi 3
asubuhi. Hii si kwamba ameachiwa huru, bali amebadilishiwa adhabu na
atatumikia kifungo chake nje, kitaalamu tunaita ‘community service’”
amesema Mboje

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top