Mahakama
ya Rufani imetupilia mbali rufaa iliyokatwa na wapiga kura wanne wa Jimbo la
Bunda Mjini Mkoani Mwanza ya kupinga ushindi wa Mbunge, Esther Bulaya katika
uchaguzi Mkuu wa Wabunge, Madiwani na Rais wa Tanzania ulifanyika Oktoba 25
mwaka 2015.
Wapiga kura hao ambao
wanampigania aliyekuwa Waziri wa Chakula, Kilimo na Ushirika na mgombea ubunge
wa CCM Jimbo la Bunda Mjini, Stephen Wasira, wapo wanne ambao ni; Magambo
Masato, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Ascetic Malagila.
Uamuzi huo umetolewa jana na Naibu Msajili wa mahakama hiyo, Elizabeth Mkwizu ambapo alisema, upande wa walalamikaji uliwasilisha hoja 10 za kupinga ushindi wa Bulaya, lakini hoja hizo hazikuwa na mashiko, hivyo zinatupiliwa mbali.
Uamuzi huo umetolewa jana na Naibu Msajili wa mahakama hiyo, Elizabeth Mkwizu ambapo alisema, upande wa walalamikaji uliwasilisha hoja 10 za kupinga ushindi wa Bulaya, lakini hoja hizo hazikuwa na mashiko, hivyo zinatupiliwa mbali.
Miongoni
mwa hoja zao ni “Stephen Wassira, hakualikwa katika mchakato wa kujumlisha
kura suala hili linaweza kuathiri matokeo ya uchaguzi kwa kushindwa kumtambua
mgombea wala chama chake,”
Baada
ya maamuzi hayo Mbunge huyo kupitia ukurasa wake wa twitter aliandika maneno
machache ambayo alimshukuru Mungu kwa kitendo cha kushinda kesi hiyo dhidi ya
wapiga kura hao.
"Wana
bunda wameshinda tena na tena, asante Mungu", aliandika Bulaya.
Post a Comment
karibu kwa maoni