0
Idadi kubwa ya tembo huuawa na majangili

Maafisa kutoka Hifadhi ya Taifa ya Garamba nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamesema kuwa Tembo 45 wameuawa tangu mwanzo wa mwaka huu. 

Maafisa hao wanasema endapo uhalifu huo utaendelea kukithiri, Tembo huenda wakapotea kabisa katika mbuga hiyo, ambayo ni moja ya maeneo yaliyo na tembo wengi zaidi barani afrika. 

Ripoti zinasema Ndovu hao huuawa na makundi ya waasi nchini DRC, wapiganaji wa kundi la waasi wa LRA kutoka Uganda, na waasi wa Sudan Kusini.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top