0



Sarah Bundala (55) amejiua kwa kujinyonga kutokana  na kutokua na uwezo wa kutorejesha pesa za mkopo alizo mdhamini rafiki yake ambae ametoroka.
Sarah akiwa ni mkaazi wa mtaa wa Tambukareli kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga.
Akisimulia kuhusu tukio hilo rafiki yake Mariam Mgaya, alisema kuwa majira ya saa nane mchana siku ya tukio alimuita ili amsindikize wakatafute pesa za kukopa, ili akarejeshe marejesho lakini walivyozunguka na kukosa ndipo akamshauri ampigie simu mume wake amsaidie kiasi hicho cha pesa anachohitaji akagoma kufanya hivyo.
 Alisema baada ya kushauriana wapi watapata pesa na kukosa majibu, marehemu alimwambia anataka kwenda nyumbani kulala kwanza na ikifika majira ya saa 10 arudi kumuona na hata watu wakimuuliza yuko wapi awaambie amelala nyumbani kwake asiwafiche na ilipofika muda huo akapokea taarifa rafiki yake amejinyonga.
Akizungumzia tukio hilo mume wa marehemu Laurent Mabina, alisema wakati akiwa bado kazini majira ya saa 9 mchana alipigiwa Simu na mke wake akimuomba Shilingi 40,000/- akamjibu kuwa anarejea nyumbani muda huo na akifika wataangalia cha kufanya lakini alipofika akakuta mkewe amejinyonga.
“Mke wangu alishawahi kukopa fedha akashindwa kulipa nikalazimika kulipa na kumuonya kwamba asijiingize tena kwenye masuala ya mikopo,huenda sababu ya mke wangu kujinyonga ni ile hofu kuwa nikirudi nyumbani nitakuja kugombana naye sababu nilishamkataza mambo ya mikopo” alisema Mabina.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea jana Ijumaa Julai 14,2017.

 

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top