0



Chama cha demokrasia na Maendeleo chadema kimemtaka rais John Pombe Mgufuli kuruhusu mikutano ya hadahara ya vyama vya siasa ili waweze kuzungumza na wananchi.
Hayo yameelezwa na afisa oganizesheni kanda ya kasakazini Ndonde Totinan wakati akizungumza leo katika mkutano mkuu wa chama hicho jimbo la Babati mjini ambapo amesema tangu kupigwa kwa marufuku mikutano hiyo wameshindwa kufanya baadhi ya mambo muhimu ikiwemo kuzungumza na wananchi na kuwaeleza mipango na mikakati waliyonayo katika majimbo.

Naye Mwenyekiti wa Jimbo la Babati mjini Hassana Madole amesema kuzuiwa kufanyika kwa mikutano ya kisiasa na kuzuia katiba kufanya kazi hivyo amemuomba rais Magufuli alegeze sharti hilo.

Chadema jimbo la Babati mjini limefanya mkutano wake mkuu na kuwakutanisha wajumbe katika ngazi zote ili kuweka mikakati ya kuimarisha chama chao.

Ikumbukwe kuwa CHADEMA ndio chama kinachoongoza katika Halmashauri ya Babati mji,Mbunge na viti vitano vya udiwani huku CCM ikiwa na viti vitano vya udiwani kati ya kata nane zilizopo katika jimbo hilo.



Nae mmoja wa wajumbe wa chama hicho kutoka kata ya Maisaka  ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Maisaka Wilson Peter Mtatiro amesema kuwa wamekuwa wakishindwa kufanya shuguli mbalimbali za kisiasa kwa kushindwa kuzungumza na wananchi na pia kupoteza wanachama.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top