Ili
kufikia adhima ya Serikali ya kutoa Elimu Bora,Wananchia wametakiwa kuendelea
kuchangia miundo mbinu ya Elimua kwa hali na Mali katika maeneo yao, ili
kupunguza upungufu wa Madarasa pamoja na Vifaa vya Elimu.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya
ya Babati Ndg Hamisi Iddi Malinga wakati alipotembelea Ujenzi wa Madarasa 4,
Offisi 2, Choo cha Matundu 12, katika shule Mpya ya Sekondari Matufa .
Aidha
Mkurugenzi huyo amewaahidi Wananchi kuwa
atatoa Bati za kuezekea Jengo hilo,
kwani lengo la Serikali nikuwawezesha Wananchi
na kuwaunga mkono katika Miradi mbalimbali ya maendeleo.
Sambamba
na hilo Mkurugenzi huyo ametembelea ujenzi wa Bweni la Kidato cha tano na Madarasa
2,pamoja na ukarabati wa madarasa 3, katika Shule ya Sekondari ya Mbugwe
iliyopo Kata ya Mwada na kutoa wito kwa Viongozi kusimamia ujenzi huo
kikamilifu.
Hata
hivyo Serikali inaendelea kukabiliana na changamoto katika secta ya Elimu kwa
kuwashirikisha Wazazi na Wananchi kuchangia kwa hali na mali Miradi ya
maendeleo katika maeneo yao.
Post a Comment
karibu kwa maoni