
Sherehe kubwa rasmi, inayotarajiwa kugharimu zaidi ya dola milioni moja za Kimarekani, itaandaliwa siku ya Jumamosi.
Rais Mugabe aliongoza Zimbabwe kupata uhuru wake mwaka 1980 na ametangaza kwamba anapanga kuwania katika uchaguzi mkuu mwaka ujao, ambapo atakuwa na umri wa miaka 94.
Mugabe alizaliwa 21 Februari, 1924.
Alifungwa jela 1964-1974 kwa kutoa "hotuba ya kuhujumu serikali"
Baada ya kuachiliwa, alisaidia kuongoza vita dhidi ya serikali ya Rhodesia
Vita vilipomalizika, Mugabe alishinda uchaguzi 1980 na akawa waziri mkuu wa Zimbabwe na akaongoza taifa hilo kama waziri mkuu hadi mwaka 1987.
Post a Comment
karibu kwa maoni