
Bw. Joshua ameandika katika mtandao wake wa kijamii kumhusu Mchungaji Penuel Mnguni, kuhudhuria ibada yake.
Gazeti la Afrika Kusini, Citizen, limemnukuu Bw. Mnguni akisema kuwa amebadilisha moyo wake, baada ya kujikuta ndani ya utata na habari zake kugonga vichwa vya habari duniani- huku akikamatwa na kuachiwa mara kwa mara:

''Nilianza kutizama runinga ya Emmanuel TV, kumsikiliza nabii TB Joshua, na nikafahamu kuwa, nilichokuwa nikifanya haikuambatana na maandiko. Nilifahamu kuwa lilikuwa shambulio. Nikaja hadi kwa TB Joshua ili anikomboe." Amesema Bw. Mnguni.
Mashtaka dhidi ya Bw. Mnguni, yaliyowasilishwa na chama cha kupambana na dhuluma dhidi ya wanyama (Society for the Prevention of Cruelty to Animals), Afrika Kusini, yaliondolewa mnamo Julai mwaka 2015, kwa kukosa ushahidi.
Post a Comment
karibu kwa maoni