0
Mwanafunzi wa darasa la tatu Daniel Agape(9) anaesoma  shule ya msingi Kwaang'w  katika Halmashauri ya Mji wa Babati anaelezea
jinsi alivyokatishwa masomo kwa kushindwa kwenda shule kutokana na ukatili
aliofanyiwa na Baba yake mzazi kwa kutokusahishiwa madaftari.


Awali Mzazi huyo Agape Majoya (34)mkazi wa Babati mtaa wa Negamsi alikua akimfungia mtoto
huyo ndani na kisha kumvua nguo na kumchapa kwa kutumia waya wa umeme hali
iliyomsababishia kuvunjika mkono wa kushoto na kuwa na maumivu makali mwilini.
Kwa upande wao majirani wa mtoto huyo katika mtaa wa Negamsi wametaka  sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho
kwa wengine.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top