0


TIMU ya Township Rollers ya Botswana imetanguliza mguu mmoja hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji, Yanga SC jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Rollers watakuwa na kazi nyepesi tu wiki ijayo watakaporudiana na Yanga mjini Gaborone ili kujihakikishia tiketi ya kwenda hatua ya 16 Bora ya mashindano, ambayo huchezwa kwa makundi, kila kundi likiundwa na timu nne.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Pacifique Ndabihawenimana aliyesaidiwa na Willy Habimana na Pascal Ndimunzigo wote wa Burundi, hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.
Na ni wageni ndio waliotangulia kupata bao dakika ya 10 tu kupitia kwa Lemponye Tshireletso kwa shuti la umbali wa mita 20 baada ya kumchungulia kipa kijana mdogo wa miaka 18, Ramadhani Kabwili na kuukwamisha mpira nyavuni kiulaini.
Yanga wakasawazisha bao hilo kupitia kwa mshambuliji wake Mzambia, Obrey Chirwa dakika ya 30 akimalizia pasi nzuri ya kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Papy Kabamba Tshishimbi.
Kipindi cha pili Yanga inayofundishwa na kocha Mzambia, George Lwandamina ilikianza vizuri na kupeleka mashambulizi mfululizo langoni mwa Rollers, lakini bahati ya kufunga bao tu ndiyo walikosa.
Pamoja na kupoteza nafasi mbili nzuri, mshika kibendera namba moja, Willy Habimana alikataa bao lililofungwa na kiungo Pius Charles Buswita akimalizia krosi ya Mwashiuya akidai alikuwa ameotea.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top