0
Mkuu wa wilaya ya Babati mkoani Manyara Raymond Mushi amewahimiza wakazi katika wilaya yake kujiunga na mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa ili kuepuka gharama kubwa za matibabu.
Amezungumza hayo wakati akikabidhi vifaa vya maabara kwenye kituo cha afya Mamire vyenye thamani ya zaidi ya shilingi million nane 8.
Kati ya hizo milioni 2.2 ni vifaa vya maabara na million 6.7 za ujenzi wa maabara nguvu za wananchi na zingine kutoka kwa wafadhili Pharmaccess international Pamoja na mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa iCHF.
Mpaka sasa mradi huu wa ICHF iliyoboreshwa imesaidia hospitali na vituo vya afya kupata matibabu ya uhakika Kwa vipimo vya kisasa pamoja  dawa kupatikana kwa wingi.
Kwa mujibu wa Meneja ICHF mkoa wa Manyara Hance John Mwankenja lengo lao  mpaka kufikia June mwaka huu wakazi wa Manyara asilimia 50 wawe wamejiunga na mfuko huu wa Bima ya afya iliyoboreshwa.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top