Rubani wa Ndege ya Kampuni ya Safari Air Link DH-SAL aina ya Cessna 206 ambayo ina uwezo wa kubeba abiria watano amefariki baada ya ndege aliyokua anairusha kuanguka katika maeneo ya Monduli, Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amesema Rubani huyo aliyetambulika kwa jina la David Mbale alikuwa akiruka kuelekea Serengeti kwa ajili kuchukua wageni. Jeshi la Polisi bado linaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.
.........................
Ndege
inayomilikiwa na kampuni ya Safari Air Link ambayo ilikuwa ikitokea
Arusha kuelekea Serengeti mkoani Mara kwa ajili ya kuchukua abiria,
ilianguka na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye ni rubani.
Ndege
hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria watano ilianguka jana katika milima
ya Monduli kijiji cha Engalaon kilichopo wilaya ya Arumeru mpakani na
wilaya ya Monduli huku chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna
(DCP) Charles Omari Mkumbo alisema kwamba ndege hiyo aina ya Cessina
206 yenye namba za usajili 5H-SAL 206 ilianza safari ya kutoka uwanja wa
ndege wa Arusha jana muda wa saa 1:05 Asubuhi ikiwa na rubani pekee na
muda wa saa 4:00 Asubuhi taarifa za kuanguka ndege hiyo zilianza
kusikika.
“Mara
baada ya taarifa hiyo muda wa saa 6:30 Mchana ndege hiyo ilionekana na
kubainika kuwepo kwa mwili wa mtu mmoja ambaye ni Rubani aliyejulikana
kwa jina la David Mbale (25) mkazi wa Dar es saalam ambao umehifadhiwa
katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru”. Alisema Kamanda Mkumbo, na
kubainisha kuwa uchunguzi wa tukio hilo utafanywa na wataalamu ili
kubaini chanzo cha ajali hiyo.
Post a Comment
karibu kwa maoni