
Aidha, katika mazungumzo hayo na kikosi cha Jeshi hilo amewasilisha ombi la kupatiwa Boti za kisasa zitakazotumiwa Jeshi la polisi katika kuimarisha doria kwenye mwambao wa bahari ya hindi ili kukomesha biashara za magendo ikiwemo ya dawa za kulevya na bandari bubu.
Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Majini la China Real Admiral, Shen Hao amesema kuwa ombi la Mkuu wa Mkoa la kupatiwa Boti za kisasa watalitimiza na kueleza kuwa wataendelea kuimarisha mahusiano ya kijeshi baina ya Tanzania na China.
Post a Comment
karibu kwa maoni