Chadema wamesema hakuna sheria yoyote inayompa Sirro mamlaka hayo na kwamba anatakiwa kuacha kutoa kauli za kuwanyamazisha.
Kauli hiyo ya Chadema, imetolewa leo na Mwanasheria wa chama hicho, John Mallya alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho.Amesema Sirro hana ubavu wa kuzuia watu wakiwamo wanasiasa kuendelea kujadili suala hilo.
“Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa haki na fursa kwa wananchi kutoa maoni na mawazo yao na kupashana habari pamoja na sheria nyingine na ibara hii ndio msingi, ” amesema Malya.
CHANZO:MWANAHALISI ONLINE
Post a Comment
karibu kwa maoni