0
Image result for polisi tanzaniaJeshi la polisi mkoani MANYARA linamshikilia mkazi wa Kijungu  wilaya ya KITETO kwa kumiliki silaha aina ya Bunduki [GOBORE] kinyume na taratibu za nchi ya Tanzania.
Mtuhumiwa anayeshikiliwa na jeshi la polisi ni Sikujua Kalulu [32] Mgogo mkazi wa kitongoji cha kona Kijungu  aliyepekuliwa nyumbani kwake baada ya polisi waliokuwa doria kupata taaifa kutoka kwa raia wema na kukuta silaha hiyo chini ya  godoro.
Mtuhumiwa huyo alipekuliwa na polisi hao majira ya saa sita mchana tarehe 26 novemba mwaka huu huku mashuhuda wakishuhudia.
Silaha hiyo ipo mikononi mwa jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi  japo uzoefu unaonyesha kuwa silaa kama hizo hutumika katika kufanyia ujangili na matukio mengine ya uhalifu.
Akizungumza na mtandao huu kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara Agustino Senga ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo anaendelea kuchunguzwa na muda wowote atapandishwa kizimbani.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara  Agustino Senga amewataka wakazi wa Manyara kutoa ushirikiano katika jeshi hilo ili kukomesha vitendo vya uhalifu.
Hata hivyo kwa sasa jeshi hilo mkoani Manyara limeendelea na doria mbalimbali mchna na usiku ili kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na watu wasio na mapenzi mema na nchi yao.
Kwa upande mwingine Kamanda Senga amesema kuwa katika kuelekea katika siku kuu za mwisho wa mwaka jeshi la polisi mkoani Manyara limejidhatiti vyema katika kupambana na vitendo vyote vya uhalifu huku akiwataka wananchi kuripoti katika kituo cha polisi pindi wanapoona vitendo vya uvunjifu wa  amani.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top