1


Wanafunzi wanaohitimu katika vyuo mbalimbali vya ufundi Stadi hapa nchini wametakiwa kutumia mafunzo wanayopatiwa katika kujiajiri.
Wito huo umetolewa na mkuu wa mafunzo Wilbert Bendera  katika mahafali ya nne kwa wanafunzi wa mwaka wa pili 168 wanaohitimu katika chuo cha Ufundi stadi Manyara [VETA] katika fani tisa.
Bwana Bendera amewataka wazazi na walezi wanaowasiamia wanafunzi hao waliohitimu kuwasaidia kupata nyenzo zitakazowafungulia njia kuweza kujiajiri.Image may contain: 1 person, smiling, standing and outdoor
Ernest Msumari na Betsheba John ni wahitimu wanaeleza kuwa baada ya kupata maarifa na ujuzi mbalimbali waliopatiwa wakiwa chuoni wataweza kujiajiri na kujitegemea.
Katika kuendeleza kilimo mkoa wa Manyara chuo hicho pia kimeandaa kozi maalumu itakayoaanza mwaka ujao..

Kwa mwakani tutakuwa na mfumo mpa wa kufundisha DUO  kwa ufadhili kutoka nchi ya Ujerumani kujifunza shuleni na eneo la kazi kulingana masomo ya mhusika.

Chuo cha VETA MANYARA ni miongoni mwa vyuo 28 vinavyomilikiwa na mamlaka ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi [VETA] kilianzishwa mwezi wa kwanza mwaka 2012 na kuzinduliwa rasmi mwezi wa nne mwaka 2012.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top