
Agizo hilo pia linapiga marufuku wanawake kupiga ngoma.
Hairuhusiwi kwa wanawake kupiga ngoma.
Hatahivyo wanaweza kushiriki katika kucheza densi za kitamaduni wakiandamana na ngoma hizo, kulingana na chombo cha habari cha AFP kilichonukuu agizo hilo.
Hilo ni jaribio la kusitisha na hatua mpya ya wanawake wa Burundi kupiga ngoma.
Kitamaduni wanawake hawakuruhusiwa kupiga ngoma nchini Burundi.
Ngoma inaonekana kama yenye umbo la mwanamke.
Agizo hilo pia linasema kuwa kundi lolote litakalotaka kupiga ngoma katika nchi za ugenini litalazimika kupata ruhusa kutoka kwa wizara.
Densi ya Burundi inatambulika na shirika la Umoja wa mataifa kuhusu Utamaduni Unesco kama urithi wa utamaduni isioonekana.
Mila hiyo inasemekana kuamsha roho za mababu na kufukuza pepo wabaya.
Post a Comment
karibu kwa maoni