0


Image result for MKUU WA WILAYA YA BABATI MUSHIMkuu wa wilaya ya Babati Raymond Mushi  amewataka wadau mbalimbali wakiwemo wazazi,walimu,viongozi  wa dini na mashirika kuelekeza juhudi zao katika kutokomeza tatizo la mimba za utotoni.
Mushi ameyasema hayo katika kampeni za kupinga ndoa za utotoni iliyoandaliwa na Shirika lisilo la serikali WORL VISION TANZANIA iliyofanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Babati jumatano ya wiki hii desemba 6 mwaka huu.
Sambamba na hayo jamii imeaswa kutokushiriki katika vitendo vinavyochochea ndoa za utotoni badala yake kuwajenga watoto katika maadili  mema ya kimwili na kiroho.
Mushi ameeleza kuwa serikali ipo tayari kushirikaina na mashirika binafisi ktika jitihada za kukabiliana na tatizo la mimba za utotoni ambalo limekuwa likikatisha ndoto zao.
mratibu wa shirika la WORLD VISION wilaya ya Babati Jesca Mnana amesema wao wamedhamiria kwa kipindi cha muda wa miaka mitano kumaliza tatizo la Mimba za utotoni kwa kutoa elimu watoto kuweza kujilinda kuepuka ndoa hizo za utotoni pamoja na kuhakikisha sera za watoto zinatekelezwa.
‘World Vision kupitia kampeni hiyo inataka kuhakikisha vijana na watoto wanapata stadi za Maisha ikiwemo elimu ya afya ya uzazi’
Kwa upande wa mratibu wa mradi wa ADP Magugu unaosimamiwa na World Vision alisema kuwa ulinzi na usalama wa mtoto ni wajibu wa kila mtu na kwamba kupitia shirika hilo wanaelimisha jamii juu yua haki,ustawi wa mtoto na wajibu wa mzazi au mlezi katika kumlea na kumlinda mtoto.
Alisema watoto wengi wanafanyiwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji na hivyo kusababisha kushindwa kufurahia utoto wao na kuwaletea madhara makubwa ikiwemo kuathiri kisaikolojia huku akisema kuwa hilo lisipokomeshwa litaongeza hali ya umaskini nchini nchini kuongezeka.
Hata hivyo katika uzinduzi wa kampeni hiyo uliowashirikisha viongozi mbalimbali wa serikali,siasa na dini ambao uliazimia kukomesha ukatili katika wilaya ya Babati kwa kutengeneza mkakati wa kamati ya ulinzi na usalama katika kata 12 kati ya  25 zitakazosaidia kutokomeza ndoa hizo.
Aidha wadau hao waliishauri serikali kubadili sheria ya ndoa ya mwaka 1971bili iendane na mazingira ya sasa na pia kuondoa mila kandamizi ambazo baadhi hulazimisha ndoa za umri mdogo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top