
Tukio hilo limetokea majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo
karibu na Grocery iitwayo Metalic Pub amabapo wawili hao wakiwa tayari wamelewa
walianza kuzozana ndipo mtuhumiwa huyo akachomoa sime aliyokuwa nayo na kumkata
kijana huyo.
Afisa mtendaji wa kata ya Galapo Dorrice Abdala akizungumza
na mwandishi wa habari hizi amekilaani
kitendo hicho huku akieleza kuwa hatua
aliyoichukua alitoa taarifa kituo cha polisi cha Gallapo.
Tukio lililotokea ni baya na ni kinyume na haki za binadamu.
Ameongeza kuwa baada ya mtu huyo kufanya tukio hilo
alikimbilia kusikojulikana
Naye diwani wa kata ya Galapo Prosper Fabian Themu alifika katika eneo la
tukio na kuwaasa wakazi wa kata yake kusheherekea siku za mwisho wa mwaka kwa
amani pamoja na kutii sheria bila
shuruti.
Msimu kama huu siku kuu vuru vurugu hizi na magrupu hayapendezi,watu wajaribu muda wote kutafuta amani ili kuepuka matukio kama hayo.
Mmoja wa mashuhuda Abdul Athuma amesema kuwa,nimefika asubuhi hapa nimekuta mtu kakatwa mkono hapa nasikia ni kijana wa mzee wa Shaa shaa aliefanya uhalifu huo.
Mganga wa kituo cha
afya Galapo amethibitisha kupokelewa kwa mtu huyo huku akieleza kuwa anaendelea
vizuri na matibabu .
Ikumbukwe kwamba jeshi la polisi mkoa wa Manyara kupitia kwa
msemaji wake Agustino Senga limesisistiza wananchi kusheherekea sherehe hizi za mwisho wa mwaka kwa amani na
utulivu na kuongeza kuwa limejipanga kukabiliana na aina yeyote ya uvunjifu wa
amani.
Post a Comment
karibu kwa maoni