0


Mashindano ya mbio za wazi Mjini Babati [BABATI HALF MARATHON] katika mbio za kilomita 5 na kilomita 21  yamefanyika leo yakiwakutanisha watoto,wanawake na wavulana.
Mshindi wa kwanza katika mbio za kilomita 21 ni Elisante Sule kutoka wilaya ya Mbulu aliekimbia kwa saa 1:08:29,wa pili ambaye ni Paskali Mombo kutoka wilaya ya Hanang-Katesh amekimbia kwa saa 1:56:54 wakati Elikarimu Japhet na kutoka mkoani Singida amemaliza mbio kwa saa 1:02:09.
Washiriki wengine na nafasi zao kwenye mabano ni Emanuel Joseph  kutoka Babati[4],Charles Sule -Mbulu[5] Musa Migire- Babati  [6],Shamba Kishinde-Babati[7],Paulo Godi –Babati [8],Eliasi Emanuel -Arusha[9] na Ginawe Gidafesta-Hanang-Katesh 10.
Mshindi wa kwanza alijichukulia shilimgi taslimu za kitanzania 50,000,wa pili 30,000 na wa tatu kanyakua shilingi 20,000.
Kwa upande wa wasichana kilomita 21 walikuwa wawili ambapo Noella Remmy ameshika nafasi ya kwanza baada ya kukimbia kwa saa 1:18:43 akifuatiwa na Paulina Hangali ambaye amekimbia saa 1:36:19.
Nao watoto walioshiriki mbio hizo kilomita 5  na muda wao ni Boay John mshindi namba moja aliekimbia kwa kukimbia kwa  14:35:07 na kupewa zawadi ya pesa shilingi 30,000, wa pili ni Remmy Israel  muda  15:17:68 kakabidhiwa shilingi 20,000 na wa tatu ni Mathayo Israel muda wake ni 15:40:50 amepewa shilingi 10,000,Athanasi Sebastian 26:08:66, [4],Rama Juma 16:33:00 [5],Paulo Wema 16:35:98 [6]na Marcell Emanuel 16:43:12 [7].
Wakati wasichana ni Joyce Petro 17:38:35,[1]Justina Melkiori 17:59:53 [2],Hadija Mohamedi  19:13:22 [3],Christina John 19:21:81 [4],Paskalina Ema 19:32:38 [5],Mery John 19:43:46 [6],Joyce Joseph 19:55:25 [7],Zanura Mohammedi 20:8:33 [8],Asha Kumba 20:35:80 [9] pamoja na Anna Martin 20:41:99 namba 10.
Hata hivyo zawadi hizo zilizotolewa ni ndogo mno ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo mshindi wa kwanza alikuwa akipatiwa hadi shilingi milioni moja na washiriki wengine kupatiwa zawadi kwa ajili ya kuwapa motisha ya kuendelea kushiriki msimu mwingine lakini kwa BABATI HALF MARATHON  2017 walioshiriki wote kuanzia namba nne na kuendelea wameambulia mikono mitupu,waswahili walisema Mikono mitupu hailambwi.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina yao baadhi ya wanariadha walioshiriki katika mbio hizo wamesema kuwa wamesononeka sana kuitwa jukwaani na kupewa mikono mitupu huku MC akitangaza kuwa ni zawadi mojawapo.Wameongeza kuwa ni vyema wangeandaliwa chochote hata kama ni kidogo wangeridhika.
Mwenyekiti wa BABATI HALF MARATHON Ali Kericho amesema hii yote imechangiwa na uongozi uliokuwepo ambao walijichagua wenyewe bila kupigiwa kura hali inayopekea mambo kwenda bila taratibu.
Mwenyekiti huyo amabye ana muda wa wiki mbili tu tangu achaguliwe anasema ilimuwia vigumu sana hadi kufika hatua ya kukata tamaa mashindano hayo kufanyika lakini akapambana na kupata msaada kutoka  Halmashauri ya mji wa Babati huku wakisaidiwa na mwenykiti Mohammedi Kibiki na kuongeza kuwa walipofika kuomba sapoti walielezwa  kuwa wamechelewa kwani kwa wadau mbalimbali yakiwemo makampuni muda wao ulishakwisha na kufunga mahesabu ya mwaka .
Akizungumza mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Babati Mohammedi Kibiki amewaasa wazazi kuwahimiza watoto wao kushiriki katika mchezo wa riadha ili miaka inayokuja Babati iweze kutembea kifua mbele kwa  kuwa na wachezaji wengi wa mchezo huo ambao umetoa ajira kwa vijana wengi.
Baadhi ya wanariadha wakubwa wakizungumza wamesema kuwa riadha imewafanya kujua nchi nyingi ambazo katika ndoto zao hawakuwahi kufikira kama wangweza kufika huko lakini kupitia riadha wameweza kufika nchi mbalimbali duniani na kupata fedha za kuendesha maisha yao.
Katibu mkuu wa Babati Half Marathon Ernest Martin alisema Babati half Marathon yanayofanyika kila tarehe 31.12 kila mwaka yanasimamiwa na chama cha riadha Babati na yamepewa Baraka zote na chama cha riadha Tanzania RT huku yakiwa na malengo ya kukuza na kuendeleza vipaji,ajira kwa vijana pamoja na kufunga na kufungua mwaka.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top