0
Anaandika Gharib Mzinga.
Image may contain: 1 person, standingWadau wote wa  kandanda nchini Tanzania wanaukumbuka mwaka 1980 kama kumbukumbu iliyobaki katika historia ya soka la Tanzania, mwaka huu ndio rasmi timu ya taifa ya Tanzania ilifuzu kucheza michuano ya mataifa huru Afrika iliyofanyika Nigeria. Michuano hiyo ya AFCON ina thamani kubwa na inashika nafasi ya pili kwa mataifa ya Africa ukiacha kombe la  dunia.    1980 taifa stars ilikua chini ya mwalimu Slawomir Wolk raia wa poland Akishirikiana vema na Joel nkaya Bendera, vichwa hivi viwili vilishirikiana kwa uwezo wao wakaifikisha taifa stars Afcon ambayo ni ndoto kubwa kwa mataifa mengi kufika hususan ya Africa Mashariki, Tanzania ilitolewa hatua ya awali kutokana na kupangwa kundi gumu zaidi likiwa na Egypt, Nigeria na Ivory coast.
walimu hawa waliweza kudhibiti na kuyaongoza vema majina makubwa katika Soka la  Tanzania, wachezaji kama Jella mtagwa wa yanga, Leodiger Tenga wa Pan Africa, Amir salim wa  coastal Union, Mtemi ramadhani wa simba, Hussein Ngulungu wa Moro united, peter Tino wa Pan Africa, Boniface mkwasa wa yanga, Othman Mambosasa wa simba na wengine, waliunganishwa na kua Tanzania.
 Ni miaka takriban 37 sasa, hakuna mwalimu mwengine au wachezaji wengine walioweza kulipa deni hilo la kuipeleka Tanzania katika michuano hiyo. Labda kikosi cha 2011 cha Jan Paulsen chini ya nahodha shadrack Nsajigwa, Kelvin Yondani, Juma nyoso, Adam nditi, John Bocco, Mrisho Ngassa, Juma kaseja kiliweza kwa namna yake kulipa deni la Kikosi cha 1974 kilichochukua ubingwa wa chalenji chini ya Sanday manara, Mohammed Bakari Tall, sembuli na wengine.  Deni limebaki kwa taifa stars hii ya sasa, kwa mwalimu na wachezaji, mujitahidi mulipe hilo deni, Joel Bendera amefariki usiku wa jumatano ya tar 6 katika hospitali ya muhimbili dar es salaam. Mwalimu wa sasa anatakiwa alipe deni la  Joel Bendera ili furaha ya watanzania irejee na isibaki simanzi kwenye mioyo pindi jina la  Slawomir Wolk na Joel Bendera likitajwa.
Waenziwe wachezaji wa zamani na kukaa nao ili kufahamu vingi kutoka kwao, hawa wataweza kutoa mwenendo mzuri wa tabia ya mchezaji, mbinu mbadala, hamasa na hata radhi zao zitasaidia kizazi hiki, hivyo  kuna haja ya kuthamini mchango wao, la sivyo tutaendelea kudaiwa ushiriki wao wa  Afcon milele. Na hapo Slawomir Wolk, Joel Bendera, na kikosi chake watabakia kua Mashujaa wa  muda wote.
#Mungu_ibariki_Tanzania
#Mungu_Mrehemu_Joel_Bendera.
Amiin.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top