Naibu waziri
mhandisi Josephat Kandege amewataka wakala wa bara bara za vijijni na mijini
TARURA kuhakikisha kuwa kazi wanazozifanya zitokane na mipango ya Halmashauri
husika.
Amesesma Lengo
la kuanzishwa kwa TARURA Sio kama chombo ambacho hakitaguswa la hasha tunataka ile hali iliyokuwa inatokana
na madiwani na wabunge kulalamika kwamba wapatiwe hata vipande vya barabara na
kujengewa makalvati ili barabara zao zipandishwe hadhi, ili ile thamani ya pesa
ionekane, na hivyo TARURA itafanya kazi sawa na TANROADS au zaidi.
Pia naibu
waziri ameongeza kwa kusema kuwa kwa sasa Babati inavutia,inatia matumani na ni salama kwa makazi hivyo kuwataka
wananchi waweke uwekezaji mkubwa kwa kuwa miundo mbinu yake ipo vizuri,hakuna
mafuriko kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
Naye Mbunge wa Babati mjini Pauline Gekul
akizungumza na Naibu waziri ofisi ya
Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Josephat Kandege ,alisema ilivyopita
V.I.T ilisaidia katika kurahisisha mradi huu wa Bara bara.
Mkuu wa
wilaya ya Babati Raymond Mushi alisema kuwa Babati ni mahali salama na sahihi
kwa kuwekeza na kwamba kilichobaki kwa Halmashauri ni kutekeleza mradi wa bara
bara uliobakia wa kilomita 4 kuhakikisha zinajengwa katika hali ya ubora kama
sehemu ya kilomita 1.6 ambayo imeshakamilika.
Kwa upande
wa meneja wa Wakala wa
Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania [TARURA] mjini Babati Mhandisi
Innocent Ambrose alisema wamepokea maelekezo ya Naibu waziri na wapo tayari
kuyafanyia kazi.
Alisema
:Awali tulikuwa tunatumia mfumo wa
Dromas yaaani tunafanya Annual Road
Inventory kila mwaka,ndipo tunapata bara bara ipi tuipe kipaumbele.
Post a Comment
karibu kwa maoni