
Ilikuwa ni
mechi ngumu sana ambayo haikuwa na utabiri kama ilivyozoeleka kwa wengi huwa
wana matokeo mapemaa.

Mchezo wa
leo ambao ni fainali ilishuhudiwa timu zote mbili zikikamiana vya kutosha mpaka
dakika 90 za kawaida za mchezo kumalizika kukiwa hakuna yeyote aliechungulia
lango la mwenzake na kulazimika waamuzi wa mchezo huo kuamua kupata mshindi kwa
mikwaju ya Penati ambayo imewawezesha Azam Fc ya Tanzania kupata mabao 4-3 URA
na kuchukua kombe hilo kwa mara ya pili Mfululizo baada ya kuchukua pia mwaka
uliopita.
Piakatika rekodi Azam FC wanatwaa Kombe la Mapinduzi kwa mara ya nne
baada ya awali kulibeba pia katika miaka ya 2012, 2013 na 2017 wakiipiku Simba
SC ya Dar es Salaam iliyotwaa mara tatu 2008, 2011 na 2015.
Yanga SC ndiye bingwa wa kwanza wa Kombe la Mapinduzi mwaka 2007 wakati timu nyingine zilizotwaa taji hilo ni Miembeni mwaka 2009, Mtibwa Sugar mwaka 2010 na KCCA ya Uganda mwaka 2014.
Jumla ya timu 11 zilishiriki michuano ya mwaka huu ambazo ni URA, Jamhuri, Mwenge, Azam na Simba zilizokuwa Kundi A na Zimamoto, Mlandege, Yanga, JKU, Taifa Jan’gombe na Singida United zilizokuwa Kundi B.
Yanga SC ndiye bingwa wa kwanza wa Kombe la Mapinduzi mwaka 2007 wakati timu nyingine zilizotwaa taji hilo ni Miembeni mwaka 2009, Mtibwa Sugar mwaka 2010 na KCCA ya Uganda mwaka 2014.
Jumla ya timu 11 zilishiriki michuano ya mwaka huu ambazo ni URA, Jamhuri, Mwenge, Azam na Simba zilizokuwa Kundi A na Zimamoto, Mlandege, Yanga, JKU, Taifa Jan’gombe na Singida United zilizokuwa Kundi B.
Magoli hayo
kwa njia ya Penalti Azam FC yamefungwa na Nahodha Himid Mao, Yakubu
Mohammed, Enock Atta Agyei na Aggrey Morris wakati Bruce Kangwa alimpelekea
mikononi mpira kipa wa URA, Alionzi Nafian na penalti za URA zimefungwa na
Charles Ssempa, Shafiq Kagimu na Jimmy Kulaba.
Wafungaji URA
ni Charles Ssempa, Shafiq Kagimu na Jimmy Kulaba.
Mchezo huo
uliohudhuriwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohammed Shein.
Pongezi
nyingi zimwendee mlinda mlango wa Azm Fc Mghana Razack Abalora aliyecheza penalti mbili
za wachezaji wa URA.
Post a Comment
karibu kwa maoni