0
Leo january 9, 2018 Muslim Hassanali ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA amehamia rasmi Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo amepokelewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philip Mangulla Pugu jijini Dar es Salaam.
Hassanali pia aligombea ubunge wa Jimbo la Ilala kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA.
Kiongozi mkubwa wa upinzani aliyejiunga na CCM leo ni Muslim Hassanali aliyekuwa mgombea ubunge Ilala kwa tiketi ya Chadema 2015 .

Pia alikuwa ni  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini  na  mmoja kati ya watia saini wa ruzuku za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

 Kujiunga kwa Hassanali ni mwendelezo wa mfululizo wa viongozi wa upinzani wakiwemo wabunge na madiwani kuondoka na kujiunga CCM.

Tayari viongozi kadhaa wakiwemo wabunge na wapinzani wamejiunga na CCM wakitokea upinzani kwa sababu tofautitofauti ikiwemo ya kuunga mkono serikali ya Rais John Magufuli.

Kiongozi huyo amepokelewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula akiwa na viongozi wengine wa CCM katika ukumbi wa Checkpoint Pugu jijini Dar es Salaam. 

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top