0


Image result for CHAKULA CHA SUMUWatu nane wilayani Kiteto mkoani Manyara wamefariki dunia,huku vyanzo vya vifo hivyo vikidhaniwa kuwa ni Uyoga sumu na nyama ya Ng’ombe yenye ugonjwa.
Wakati wakazi hao wakiripotiwa kufariki dunia, zaidi ya ng’ombe 6,000 wilayani humo wamekufa.
Akizungumza na WALTER HABARI KWA NJIA YA SIMU, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto,Tumaini Magessa amesema mpaka sasa idara ya mifugo wilayani humo imewasiliana na wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) ambao wanaendelea na uchunguzi.
Dc.Magessa ameeleza kwamba wataalamu hao kwa kushirikiana na wengine wa Wizara ya Afya wameshachukua sampuli kutoka kwa watu waliofariki, ng’ombe waliokufa na Uyoga kwa ajili ya kufanya uchunguzi.
Aidha amesema  Majina ya waliofariki dunia bado hayajapatikana ila wawili walifariki katika Kata ya Kiperesa, wanne katika Kijiji cha Emat, Kata ya Magungu na wengine wawili bado hawajajua walikuwa wakazi wa kijiji kipi.
Hata hivyo Magessa Alisema, Baada ya ukame, mvua kubwa ilinyesha na majani mapya kuota,ambapo wafugaji  wanasema huenda Ng’ombe hao wamekufa kutokana na kula nyasi hizo ambazo bado hazijakomaa.

Amesema mizoga ya Ng’ombe waliokufa walikutwa maeneo tofauti, mingine ikiwa barabarani na porini.
Mkuu huyo wa wilaya amewataka wananchi wa Kiteto kuendelea kuchukua tahadhari wakati ambapo wanasubiri majibu ya uchunguzi wa wataalamu.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top