0


Katika kata za Endasak, Wareta, Dawar, Dirma na Gendabi ambako Usajili unaendeshwa na Ofisi ya Usajili ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ya wilayani Hanang` kwa kushirikiana kwa karibu na ofisi ya Usajili ya wilaya ya Hanang`.

Katika hali isiyo ya kawaida umati mkubwa wa wakazi wa kata hizo wamejitokeza Kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa jambo ambalo si la kawaida kwani kwa kipindi cha majira haya wengi huwa kwenye mawindo na kutafuta malisho kwa mifugo yao na baadhi yao wachache huwa kwenye shughuli za kilimo.

Baadhi ya wananchi wa kata hizo walipohojiwa kwa nyakati tofauti wameonyesha kuelewa umuhimu na ulazima wa wao kujitokeza wasajiliwe kwani wameelezwa na watendaji wao wa Kata na Wenyeviti Serikali za vijiji kuwa kila mkazi mwenye umri wa miaka 18 na zaidi anatakiwa Kujisajili ili Serikali iweze kutambua wananchi wake wanaoishi wilaya ya Hanang jambo litakalowasaidia katika utoaji huduma kwa wananchi wake ikiwemo umiliki wa ardhi bila kubugudhiwa.

 Mzee Paskali Gway Pamy wa Kijiji cha Huwanemba Kata ya Dirma wilayani Hanang` amesema imemlazimu kuachia watoto mifugo yake ili aweze kukusanya familia yake yote (wenyeumri wa miaka 18 na zaidi) wakiwemo wake zake ili Wasajiliwe na kupata Kitambulisho cha Taifa.

Naye Afisa Msajili Wilaya ya Hanang`Ndg. Amwesiga K. Bandio amekiri kuwepo kwa mwitiko mkubwa wa wananchi katika vituo jambo linalotia moyo.

Inaonyesha kwa sasa wananchi wengi wamehamasiska sana na kwa sehemu wameshaelewa umuhimu wa kuwa na Kitambulisho cha Taifa.Ndg. Bandio ameushukuru uongozi wa wilaya kwa kutoa ushirikiano wa karibu ikiwa ni kutoa maelekezo kwa watendaji kuhakikisha wanaelimisha na kuhamasisha umma katika Kata, vijiji na vitongoji vyao wajitokeze kusajiliwa kwa wakati.  


 Aidha ameeleza kwa sasa Ofisi ya Usajili wilaya anayoisimamia imeshakamilisha Usajili katika kata za Katesh, Ganana, Jorodom, Dumbeta, Mogitu, Nangwa na Endasak.
Afisa Habari wa NIDA Bi Agnes Gerald akitoa maelekezo kwa mwananchi alipokuwa katika zoezi la Uandikishaji wilaya ya Hanang mkoani Manyara.      

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top