Mama wa Mkuu wa mkoa Arusha, Mrisho Gambo anatarajiwa kuzikwa Uru mkoani Kilimanjaro baada ya mwili wake kurejeshwa nchini.
Katibu
Tawala Mkoa Arusha, Richard Kwitega alisema hayo wakati akizungumza
katika dua maalum leo, Aprili 14, iliyofanyika nyumbani kwa Mkuu wa
Mkoa.
Kwitega amesema, mwili wa marehemu Rehema Momburi, unatarajiwa kuwasili Jumanne kutoka nchini India.
Kwa mujibu wa ratiba, mazishi yatafanyika Alhamisi ya wiki ijayo.
Viongozi
mbalimbali wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa, umoja wafanyabiashara,
wakurugenzi, mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema na viongozi wengine
kadhaa walihudhuria.
Post a Comment
karibu kwa maoni