0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli leo Aprili 15, 2018 amefanya uteuzi wa Majaji 10 wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali, Naibu Mkurugenzi wa Mashitaka, Wakili Mkuu wa serikali na Naibu Wakili Mkuu wa serikali.
Aidha, Dkt. Magufuli amefafanua kuwa amefanya uteuzi huo wa Majaji wa Mahakama Kuu kwa lengo la kujaza nafasi za Majaji waliostafu na amefanya uteuzi wa Wakili Mkuu wa serikali na Naibi wake kwa lengo la kuhakikisha ofisi za Mwanasheria Mkuu wa serikali, Mkurugenzi wa Mashitaka na Wakili wa Mkuu wa serikali zinafanya kazi vizuri zaidi katika kushughulikia masuala ya Mahakama.
Kwa habari kamili mtazame hapa chini Rais Magufuli akizungumza juu ya uteuzi huo.



Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top