0

Image result for MILIMA WA MAWE 
Wakaazi wa kijiji cha Kiongozi kata ya Maisaka mjini Babati mkoani Manyara  wamekataa maadhimio ya Halmashauri ya Kijiji katika kikao kilichofanyika tarehe 12 mwezi wa nne mwaka 2018 chini ya mwenyekiti wa Kijiji hicho Thomas  Lohay  kuuza mlima kwa mkandarasi Rock Tronick.
Wamesema kuwa kutokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi mbalimbali ya kijiji,wanahofia hata fedha zitazotokana na mlima huo hazitowasaidia hivyo hawaoni haja ya kuuzwa na kumueleza mkurugenzi kuwa watafute maeneo mengine ili nao wanufaike.
Wakieleza malalamiko hayo kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Fortunatus Fwema katika mkutano mkuu wa Kijiji   wameaanisha miradi mbali mbali ambayo haiendani na kiwango cha fedha zilizotumika wakitolea mfano choo cha shule ya msingi Kiongozi kichogharimu shilingi million 9,978,000.
Baada ya kusikiliza malalamiko ya wananchi hao, mkurugenzi aliunga mkono hoja hizo kwa ueleza kuwa mlima huo haotouzwa.
Akizungumzia kuhusu suala la choo kujengwa chini ya kiwango amesema atawaagiza wataalamu ili kuweza kubaini kama kiasi kilichotumika kinaendana na ubora wa choo hicho.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top