0

Afisa Msajili Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Ndg. Godwill Mwamanga akizungumza na wanakijiji wa kijiji cha Sanganjelu, wilayani Gairo akifurahia taarifa ya maendeleo ya mwitikio wa wananchi Kushiriki Usajili ambapo aliarifiwa na Mwenyekiti wa kijiji hicho kuwa  mwitiko wa wananchi ni mkubwa.

Afisa Msajili wa ofisi ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wilaya ya Gairo mkoani Morogoro Ndg. Godwill Mwamanga ameeleza kuwa katika wilaya anayoisimamia zoezi la Usajili linaendelea vizuri kutokana na wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi jambo linaloonyesha matokeo chanya (asilimia kubwa) kufikiwa kwa NIDA kuweza Kusajili idadi ya wananchi wenye umri wa miaka 18 na zaidi kama ilivyo lenga.
Akizungumza wakati anatoka kituoni baada ya Kusajiliwa, Bi Fatma Mhando ameeleza amejitokeza na kuwa mstari wa mbele kushiriki Usajili kutokana na kutofanikiwa kupatiwa mkopo baada ya kutokuwa na Kitambulisho cha Kumtambulisha hivyo ‘nisingependa nifanye makosa tena kwa kupuuzia fursa hii kwani ninaweza kukosa fursa nyingi mbeleni za kuniinua kiuchumi n.k iwapo sitakuwa na Kitambulisho cha Taifa.

Aidha Ndg. Mwamanga ameeleza kuwa zoezi katika wilaya ya Gairo linatakiwa kufanyika katika kata zote 18 ambapo hadi sasa wameshakamilisha katika kata  6: Msingisi, Rubeho, Chanjale, Iyogwe, Italagwe na Mkalama. Kata mbili za Madenge na Leshata zoezi la Usajili linaendelea na kutarajiwa kukamilika mwishoni mwa wiki ili kutoa fursa kwa wananchi wa kata za Chakwale, Kibedya, Idibo, Nongwe, Mandege, Chagongwe, Ukwamani, Magoweko, Ngiloli na Gairo ambazo bado kufikiwa kupata fursa hiyo.
Wananchi wa kijiji cha Kinyolisi wakisikiliza maelekezo ya utaratibu wa Kusajiliwa kutoka kwa Mwenyekiti (katikati) uliopangwa ili kila mwananchi anayefika katika kituo hicho cha Usajili cha kijiji cha Kinyolisi asajiliwe kwa lengo la kupatiwa Kitambulisho cha Taifa. Aidha Mwananchi mwenye fulana ya kijani kulia amesitisha kuendelea kusuka na kukimbilia Kituo cha Usajili ili asikilize maelekezo na kushiriki zoezi hilo kutokana na kutambua umuhimu wake kwa maendeleo yake kama mwananchi wa Tanzania.
Maafisa Usajili Wasaidizi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiendelea na Kusajili wananchi wakazi wa kijiji cha Kilama kata ya Iyogwe wilaya ya Gairo mkoani Morogoro katika kuingiza taarifa zao kwenye mfumo. Wananchi wengine pichani wakiwa wameketi wakisubiri zamu yao ifike na kushoto Ndg. Ally John akiweka saini ya kielektroniki kwenye mashine ya BVR.
 
Afisa Msajili wa ofisi ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wilaya ya  Gairo mkoani Morogoro akizungumza na  baadhi ya viongozi na wasimamizi wa kijiji cha Ngayaki kata ya Leshata juu ya maendeleo ya zoezi na changamoto zilizopo ili zitatuliwe mapema alipofanya ziara kijijini hapo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top