0



Shule ya msingi komoto iliyopo mtaa wa Komoto halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa matundu ya vyoo,ofisi ya walimu na nyumba za walimu.


Akizungumza na redio manyara  mapema leo ofisini kwake mkuu wa shule hiyo mwalimu Eroyano ameeleza kuwa licha ya changamoto hizo pia wanafunzi hawapati chakula cha mchana shuleni hapo  kutokana na wazazi kuwa na muamko mdogo katika kuchangia hali inayoilazimu shule kuwaruhusu wanafunzi wakale majumbani wakati wa mchana na kurudi shuleni.


Mkuu huyo ameitaka serikali ya mtaa wa Komoto na Halmashauri ya mji kwa ujumla kuweza kutatua changamoto hizo mapema ili wanafunzi waweze kupata elimu katika ubora na kuwapa walimu hari katika kufundisha.


Katika hatua nyingine Eriyano ameelezza kuwa katika shule yake wanafunzi 47 waliosajiliwa kwenye baraza la mitihani kufanya mtihani wa darasa la saba ni mwanafunzi mmoja mvulana  ambaye alitoroka nyumbani kwao tangu mwezi march mwaka huu na kwenda kusikojulikana.

Mkuu huyo ameeleza kuwa pia wanakabiliwa na uhaba wa ofisi za walimu hali inayowalazimu kutumia moja kati ya madarasa kama ofisi huku kukiwa miundo mbinu chakavu ya vyoo kwa upande wa wavulana.

Naye mwalimu Nuru amekiri kuwepo kwa changamoto hizo shuleni hapo na kuitaka serikali iweze kuwatatulia kwa haraka zaidi.

Mapema mwaka huu Fedha za ruzuku zilizotolewa na serikali kwa ajili ya maendeleo ya shule za msingi na sekondari ikiwemo malipo ya ada mkoani Manyara,ambapo ilionekana kuzua utata wa matumizi yake hususani katika shule za msingi kutokana na mahitaji mengine kukwama hasa yale yaliyokuwa yakitegemea mchango wa jamii.

Utafiti wa hivi karibuni ulibaini  changamoto za matumizi ya fedha hizo kuwa  ziko katika shule za msingi huku sekondari za kutwa zikikabiliwa na changamoto ya wazazi kugomea mchango wa chakula.

Mkoa wa Manyara wenye shule za msingi 619 zenye wanafunzi 246.000, zimepatiwa ruzuku ya zaidi ya shilingi  295,778,000/=

 Na zaidi shilingi 293,748,000/= zikipelekwa kwa shule za sekondari 135 zenye idadi ya wanafunzi 46,600.

Katika moja ya shule ya Msingi Komoto, iliyoko mjini Babati ambayo imepokea mgao wa zaidi ya shilingi laki mbili kwa kipindi cha January hii, imeonekana fedha hizo kutokidhi mahitaji mengine.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top