0

Waziri wa katiba na sheria Dr. Harrison Mwakyembe amekanusha juu ya minong'ono na taarifa zilizosambaa nchini na nje ya nchi kuwa serikali ya awamu ya tano imekwamisha mchakato wa katiba mpya na kuwataka wadau na wasomi kuacha kusambaza uvumi huo.

Ikiwa ni mwezi mmoja tangu rais Magufuli wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari kusema kuwa kwa sasa anachofanya ni kuinyoosha nchi na kujenga uchumi hivyo mchakato wa katiba usubiri, kauli hiyo iliibua hoja mbalimbali huku wengine wakisema mchakato huo wa katiba sasa umekwama, waziri Mwakyembe anafafanua.
Kauli hiyo inakuja ikiwa ripoti ya utafiti juu ya uelewa wa wananchi kuhusu katiba iliyotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya OSIEA ikishirikiana na mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam ikionesha kuwa asilimia 50 ya watanzania hawaijui katiba ya sasa ya mwaka 1977, asilimia 74 hawajui inapatikana wapi wakati asilimia 14 hawajui kama kuna katiba.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top