
Kambi hiyo ya kijeshi ipo katika eneo la jimbo lililojitangazia uhuru wake la Puntland.
Mwaandishi mmoja pia wa VOA ameandika katika mtandao wake wa kijamii wa tweeter kuhusiana na shambulio hilo.
Utawala huko Puntland umethibitisha kutokea kwa shambulio hilo lakini unapinga idadi ya waliouwawa.
Duru zasema kuwa shambulio hilo la mapema Alhamisi asubuhi, lilitokea karibu na milima ya Galgala, ambao hapo awali ilikuwa ngome ya wapiganaji wa al-Shabab katika jimbo hilo la Puntland.
Mwaandishi wa BBC wa idhaa ya Kisomali Jiijini Nairobi Mohammud Ali ambaye anafuatilia taarifa hiyo, amesema kuwa jimbo la Puntland limekuwa likikumbwa na mashambulio ya mara kwa mara kutoka kwa al-Shabab, lakini hili la sasa limetajwa kuwa baya zaidi katika siku za hivi karibuni.
Post a Comment
karibu kwa maoni