1.
Mheshimiwa Spika, naomba
kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu lipokee, lijadili na kupitisha Makadirio ya
Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2017/18. Bajeti hii inawasilishwa kwa
kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977,
Ibara ya 137 ikisomwa pamoja na Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015 kifungu
cha 26.
2.
Mheshimiwa Spika, pamoja
na hotuba hii, ninawasilisha vitabu vinne vinavyoelezea kwa kina makadirio ya
Bajeti kwa Mafungu. Kitabu cha Kwanza ni Makadirio ya Mapato; Kitabu cha Pili
ni Makadirio ya Matumizi ya Kawaida kwa Wizara, Idara zinazojitegemea, Taasisi
na Wakala za Serikali; Kitabu cha Tatu ni Makadirio ya Matumizi ya Kawaida kwa
Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa; na Kitabu cha Nne ni
Makadirio ya Matumizi ya Maendeleo kwa Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za
Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, upo
Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2017 pamoja na Muswada wa Sheria ya
Matumizi ya Serikali wa mwaka 2017 ambayo ni sehemu ya Bajeti hii.
3.
Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi
Mungu kwa baraka na amani anayoendelea kuijalia nchi yetu na pia kwa
kuniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha Bajeti ya Serikali
kwa mwaka 2017/18.
4.
Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee napenda nichukue fursa hii
kumshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini katika dhamana hii kubwa ya
kuongoza wizara nyeti ya Fedha na Mipango. Aidha, ninamshukuru sana kwa
kuniongoza na kunitia moyo pale mawimbi yalipozidi kuwa makubwa. Maneno yake
mazito kwamba aliniteua ili nipigwe mawe badala yake na badala ya Watanzania
maskini na kuwa nimtegemee Mungu daima, yamekuwa ndiyo nguvu yangu katika kazi.
Vile vile, nampongeza Mheshimiwa Rais pamoja na wasaidizi wake wakuu,
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania na Mbunge wa jimbo la Ruangwa kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya
ya kutuletea maendeleo Watanzania wote.
5.
Mheshimiwa
Spika,
naomba pia kuwapongeza viongozi wakuu wa mihimili ya dola, nikianza na wewe
mwenyewe Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa jimbo
la Kongwa, na Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mbunge) Naibu Spika. Ninawapongeza
kwa umahiri na busara zenu katika kuongoza Bunge hili. Vile vile, ninawapongeza
kwa dhati Mheshimiwa Profesa Ibrahim Juma, Kaimu Jaji Mkuu, kwa kuongoza vyema
mhimili wa mahakama katika kutoa haki.
==>Endelea Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>
==>Endelea Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>
Post a Comment
karibu kwa maoni