MKURUGENZI
Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Kanda ya Afrika Mashariki,
Dkt. Nyamajeje Weggoro, amewataka wanafunzi 45 kutoka Tanzania, Kenya, Uganda na Ethiopia,
wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela cha Sayansi na Teknolojia
kilichoko mkoani Arusha, kusoma kwa bidii na maarifa ili waweze kuzisaidia nchi
zao kuinua sekta ya viwanda kwa njia ya utafiti na ubunifu wa teknolojia
mbalimbali
Dkt.
Weggoro ametoa rai hiyo alipotembelea Chuoni hapo ili kuangalia utekelezaji wa
programu ya miaka mitano ya kuboresha masuala ya rasilimali watu inayofadhiliwa
na Benki yake kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 8.2
Alisema
kuwa Benki yake imeamua kuwekeza fedha nyingi katika eneo la Sekta ya elimu ya
juu katika nyanja ya ufundi ili kuwapata vijana wa kutosha watakaoziba pengo
lililopo na kuweka misingi mizuri ya maendeleo ya baadae hasa katika matumizi
ya teknolojia na sayansi.
“Nimefurahi sana kuona wanafunzi wanasoma na
wana ari kubwa na kwamba fedha tulizozitoa zinatumika vizuri, tunadhani hata
baada ya mradi huu wa miaka 5 kukamilika,
Benki itaweza kusaidia zaidi ufadhili wa fedha na vifaa” Alisema Dkt. Weggoro.
Kaimu
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela, Prof. Joram
Buza, ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB kwa ufadhili huo, hatua iliyoongeza
udahili wa wanafunzi katika chuo hicho.
“Mwaka
wa masomo wa 2014/2015, Chuo kilidahili wanafunzi 7 pekee kutokana na
changamoto wafadhili lakini baada ya ufadhili wa AfDB na Benki ya Dunia, wanafunzi
wameongezeka hadi kufikia 135 jambo linalotia matumaini” alisema Pro. Buza.
Bi.
Mwanaisha Mkangara na Bw. Alexander Mzura, wanaosomea shahada ya uzamivu katika
masuala ya uhandisi na mifugo, kupitia ufadhili wa AfDB, wamesema kuwa masomo
yao yatawaongezea ujuzi wa namna ya kufanya utafiti wa kihandisi na kuvumbua
chanjo mbalimbali za mifugo.
AfDB
inafadhili wanafunzi 45 ambapo 42 kati yao wanatoka Tanzania, huku
Uganda, Kenya na Ethipia zikitoa mwanafunzi mmoja mmoja.
Post a Comment
karibu kwa maoni