0


Basi la kampuni ya Sharon lenye namba za usajili T 349 lililokuwa litatoka Dodoma kwenda Arusha, limepinduka eneo la mabanzini-Bohay mjini Babati na kusababisha vifo vya watu wawili huku wengine wakijeruhiwa.

Majeruhi wa ajali hiyo walipelekwa hospitali ya Mrara mjini Babati kwa matibabu zaidi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara Francis Masawe akizungumza juu ya ajali hiyo amesema kondakta na mtoto mdogo ndiyo walifariki huku 11 wakijeruhiwa.

Hata hivyo waliofariki bado hawajafamika kwa majina.

Chanzo cha ajali hiyo ni kona kali zilizopo kwenye bara bara bara hiyo inayofanyiwa matengenezo.

Shuhuda wa karibu katika ajali hiyo aliyejitambulisha kama Toto Wa Bonga anasema ‘Nilifika kama dakika kumi baada ya ajali ni uzembe usio na na kiwango baada ya kupata Chai Mjini Babati dereva alimpa gari konda aliendeshe baada ya kumaliza msitu wa Haraa kona ya kwanza kali ukitokea Boay ikamshinda gari ilikuwa mbio sana wakati wa kukata kona matairi ya upande moja yaliinuka na kupoteza mwelekeo na kuanguka konda mwenyewe amekufa dereva amekimbia mimi nilikuwepo hadi police kutoka kituo kidogo cha Bonga alipofika akibebwa na pikipiki hayo ndiyo mapokeo kutoka kwa wasafiri ni bora uchunguzi uanzie hapo.”alisema shuhuda huyo.

Aidha kamanda amesema  atazungumza na mamlaka zinazohusika na kutoa vibali ili waizuie bara bara hiyo kutumika kwani bado kwa sasa haipo vizuri kwa magari kupita haswa ya abiria.

Katika hatua nyingine ameuambia mtandao huu kuwa ajali ndani ya mkoa wa Manyara zimepungua kwa kiwango kikubwa bila kutaja ni kwa asilimia ngapi.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top