0






Wakazi wa Mkoa wa Manyara na viunga vyake wametakiwa
kujitokeza kupokea mwenge pindi unapofika katika maeneo yao ili kupata ujumbe
wa mwenge kwa mwaka 2017.
Akitoa ratiba ya mapokezi ya mbio za mwenge mkoa wa Manyara
mratibu wa Mwenge kwa mwaka 2017 Lucia Vitalis  Kamafa  amesema utapokelewa Wilayani Mbulu  Septemba 8 na kukamilisha ratiba hiyo wilayani
Simanjiro septemba 14 na hatimaye kuukabidhi mkoa wa Kilimanjaro katika wilaya
ya Hai.
Akizungumza na Redio Manyara Kamafa wa mwenge mkoa wa
Manyara kwa mwaka huu  Lucia Vitalis
Kamafa  ameeleza kuwa mbio za mwenge kwa
mwaka huu imebeba ujumbe unaoendana na azma ya ya serikali ya uchumi wa  viwanda inayosema  shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa Maendeo
ya nchi yetu.


Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top