Dokta
Mpango amesema kuwa kiwango cha mtaji ambacho Serikali ya Uingereza
imewekeza nchini hadi sasa ni Paundi bilioni 2.5 lakini kwa upande wa
biashara kati ya nchi hizo mbili, hali si nzuri.
"Mwaka
2015 Tanzania iliuza nje bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani
milioni 22.5 na kununua bidhaa kutoka Uingereza zenye thamani ya Dola
milioni 150, kiwango ambacho ni kidogo sana na tunahitaji kufanya
biashara zaidi" Alisisitiza Dkt. Mpango.
Dkt.
Mpango alitoa wito kwa Serikali ya Uingereza kuwekeza zaidi katika
viwanda vitakavyoongeza thamani ya bidhaa mbalimbali ikiwemo kujenga
viwanda vya kutengeneza matrekta na zana nyingine za kilimo, kusindika
bidhaa za mazao ya wakulima pamoja na kuwekeza katika sekta za kuongeza
thamani ya madini na nishati ya umeme.
Dokta
Mpango aliwaeleza Wabunge hao kwamba hivi sasa Serikali imepiga hatua
kubwa kiuchumi na kuishukuru Uingereza kwa mchango mkubwa inaoutoa
kusaidia Elimu, Lishe, Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma na afya
kwa upande wa lishe, uwekezaji ambao kwa pamoja umefikia zaidi ya paundi
milioni 180.
Kwa
upande wake, kiongozi wa Wabunge watano waliomtembelea Waziri wa Fedha
na Mipango, Mheshimiwa David Linden, amesema wamefurahishwa na namna
Tanzania inavyopiga hatua kubwa kimaendeleo na kudhibiti vitendo vya
rushwa.
Wabunge hao wapo nchini tangu Jumapili iliyopita na wanatembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Serikali ya Uingereza.
Post a Comment
karibu kwa maoni