Klabu ya soka ya Majimaji ya mkoani Ruvuma imejinasibu kuwafunga mabingwa watetezi wa VPL Yanga kwenye mchezo wao wa kesho.
Majimaji
kupitia kwa mjumbe wake wa kamati ya utendaji Salum Masamaki wamesema
wamejiandaa vyema chini ya mwalimu Habib Kondo na wanaamini watapata
ushindi katika mchezo wao wa kwanza kwenye uwanja wao wa nyumbani.
"Tumejiandaa vyema na mchezo
tutaifunga Yanga bila shida kwasababu timu yetu iko vizuri ndiyo mana
tumetoa sare moja na kupoteza mchezo mmoja lakini michezo yote tumecheza
ugenini", amesema Masamaki.
Katika hatua nyingine Masamaki
amethibitisha kuwa kocha wao Kally Ongala hayupo na timu kwasababu
mkataba wake unamalizika mwezi Oktoba hivyo bado anaongea na wadhamini
ambao ni GSM ili kuona kama ataongeza mkataba.
Majimaji ipo nafasi ya 12 kwenye msimamo
wa VPL ikiwa na alama moja baada ya michezo miwili na itakuwa
nyumbani kesho kucheza na Yanga kwenye raundi ya tatu.
Post a Comment
karibu kwa maoni