Onyo hilo
limetolewa na Afisa taaluma shule za sekondari
mkoa wa Manyara Lago Sillo wakati akizungumza na wazazi na wanafunzi
kwenye mahafali ya darasa la saba na kidato cha nne katika shule ya Rift Valley
Babati.
Sillo
amewataka watumishi hao wa kiimani kufanya kile walichokusudia kuwafikishia
wanafunzi hao, na sio kushawishi wanafunzi kuachana na imani walizonazo kwani
jambo hilo linaweza kuleta taswira nyingine baina ya dini.
Kwa upande
wake mkurugenzi wa Shule ya msingi na Sekondari Rift Valley Babati ndugu
Henrisalus-Laus Mallya amewataka Wazazi na walezi wa watoto waliohitimu darasa la saba na
wanaotajia kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu wametakaiwa kuwa karibu
na watoto wao ili wasijiingize katika vishawishi na makundi mabaya ili kufikia
malengo yao.
Aidha amempongeza
mkurugenzi wa shule hiyo ambae pia anazo shule nyingine mkoani kilimanajro
pamoja na vyuo vya ualimu kwa jitihada alizoonyesha katika kuwekeza kwenye
Elimu, akiwataka na wengine kuiga mfano huo.
Akizungumzia
ufaulu amesema kama shule imeshindwa kushindana
kimkoa haina haja ya kushindana na wengine wanaofanya vizuri ila ijipange upya.
Naye mwalimu
mkuu wa shule ya Sekondari Rift Valley Babati Dadly Wilfredy Mallya
akizungumzia suala la uwepo nidhamu mbaya kwa baadhi ya
wanafunzi amesema kwa kiasi
kikubwa inachangiwa na utandawazi.
Mallya
amewaomba wazazi washirikiane na walimu ili kuweza kuwajengea nidhamu bora wanafunzi
pindi wanapokuwa nymbani na shuleni pia.
Historia ya
shule ya Msingi na Sekondari Rift Valley
Babati ilianzishwa rasmi mwaka 2003 ikiwa na wanafunzi 21 lakini mwaka 2012 ikaingia
kwa msimamizi mwingine na katika mwaka huo shule iliendelea kupata wanafunzi na
mpaka sasa ina kuna wanafunzi 353.
Kwa mahafali
ya jumamosi ya leo septemba 30 2017, kwa
darasa la saba ni mahafali ya tisa na kwa kidato cha nne ni mahafali ya nne.Shule
ipo Mtaa wa Muruki,kilomita 2 tu kutoka stand ya mabasi Babati,ni shule ya
kutwa na Bweni yenye michepuo ya Sayansi,Biashara na Sanaa.
Post a Comment
karibu kwa maoni