0
#Anaandika Suleiman Ussi kutoka Zanzibar.
Ligi kuu soka ya Zanzibar imeendelea tena leo kwa kupigwa michezo miwili majira ya saa8 za mchana CHARAWE wamekubali kipigo cha mara ya pili cha mabao 4-0 dhidi ya timu ya KIPANGA  charawe wanaonekana bado kuwa wageni wa ligi kuu ya soka ya Zanzibar.

Mchezo wa pili umepigwa majira ya saa10 za jioni kati ya timu ya KILIMANI CITY wakioneshana kazi dhidi ya timu ya KMKM na katika mchezo huo timu ya  kmkm wakaibuka na ushindi wa bao 3-0 dhidi ya timu ya kilimani city  .

Ligi  kuu ya zanzibar itaendelea tena siku ya kesho kwa kupigwa mchezo mmoja tu majira ya saa10 za jioni BLACK SAILOR vs JAN’GOMBE BOYS ..

 ZFA wilaya ya mjini imeanzisha darasa maalumu la kuwafunza uwamuzi vijana wadaogo wenye umri kuanzia miaka 13 akizungumza na kipindi hiki mkufunzi huyo ambae pia ni katibu wa waamuzi Ramadhani ibada kibo amesema vijana hao wadaogo wanapopewa mechi kubwa kuchezesha wanajifariji sana na kusema vijana hao pia wameshachezesha mashindano ya Rulingi stone huku Tanzania bara huku akiwata vijana wengine pamoja na wanawake kujifunza suala zima la uwamuzi ,,    
Baada ya siku ya jana kumalizika kwa zoezi zima la upitishaji kwa madaraja ya vijana  wilaya ya mjini timu mbali mbali zimeanza maandalizi ya mazoezi ya ligi za Jivanili, Junio ,na central kipindi hiki kilifanikiwa kuzungumza na kocha wa Jivanili wa timu ya River side  Hafidhi amesema timu yake msimu huu wamejianda kwa kuchukua ubingwa pia ametoa changamoto mbali mbali zinazowakabili katika ligi hizo za vijana  ni ukata wa wazamini pamoja na zawadi.

 Baada ya siku ya jana timu ya kwerekwe city inayoshiriki ligi daraja la pili taifa kutoka suluhu ya kufungana bao 2-2 didi ya timu ya Zantex  inaendelea na mazoezi makali ya kujianda na mchezo wao ujao dhidi ya timu ya Bweleo katibu mkuu wa timu hiyo ya kwerekwe city mussa mzirai amesema mapungufu yaliojitokeza jana watahakikisha wanayafanyia kazi ili timu yao ifanikiwe kushinda katika michezo ijayoo..

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top